Tundu Lissu
Na Mwandishi Wetu/ Mara Online News
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tanzania Bara, Tundu Lissu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho - za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, utakaofanyika mjini Tarime, mkoani Mara kesho Novemba 21, 2024.
Hiyo ni kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na ofisi za CHADEMA Wilaya ya Tarime na Kanda ya Serengeti inayoundwa na mikoa ya Mara, Simiyu na Shinyanga.
Kampeni za uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa zinatarajiwa kuhitimishwa Novemba 26 ili kupisha uchaguzi wenyewe uliopangwa kufanyika nchini kote Novemba 27, 2024.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Biteko awatajia wananchi 'viongozi wa maendeleo' akizindua kampeni za CCM Mara
>>Barrick yatunukiwa tuzo ya kudhamini mkutano wa kimataifa wa madini
>>Mfanyabiashara wa Tanzania Nyambari Nyangwine sasa kuwekeza Uganda
>>Kamati ya Rufani Tarime yarejesha wagombea 100, CHADEMA, ACT Wazalendo waipongeza
No comments:
Post a Comment