NEWS

Friday 6 September 2019

TARIME KUWEKEZA KATIKA VIWANDA VYA KAHAWA

              



Na Mwandishi wetu,
Halmashauri ya Wilaya ya Tarime imepanga kuendelea kuwekeza  katika viwanda  vya kukoboa kahawa mbichi  ikiwa ni sehemu ya  juhudi za kutekeleza  sera ya uchumi wa viwanda  .
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Silvanus Gwiboha amesema  hayo leo katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo .
Aidha Gwiboha ambaye ni Mkuu wa Idara ya kilimo katika Halmashauri hiyo amesema Halmashauri wanaendelea kusimamia uanzishwaji  wa mazao mapya ya biashara ya chai na pamba katika vijiji mbalimbali.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages