NEWS

Thursday 18 July 2019

MWALIMU MKUU WA SHULE YA SEKONDARI ASHAMBULIWA NA MAJAMBAZI NYUMBANI KWAKE TARIME, TATIZO LA UMEME LAKWAMISHA MATIBABU YAKE KWA ZAIDI YA SAA MOJA

SACP Henry Mwaibambe

Na mwandishi wetu, Tarime
Mkuu wa shule ya sekondari ya Kenyamanyori Zakaria Kabengo jana usiku alishambuliwa vibaya na majambazi waliovamia nyumbani kwake Rebu Majengo  mapya  katika Mji wa Tarime Mkoani Mara.
Hata hivyo mwalimu huyo alikosa matibabu kwa zaidi ya saa moja katika hospitali ya Wilaya ya Tarime kutokana na  ukosefu wa umeme na mafuta ya jenereta.
“ Majambazi hawa waalinza kunishambulia  leo majira ya saa tatu usiku  baada ya kuona mmoja wao anamlika  tochi, nilipohoji wewe  ni nani walianza kunikatakata mapanga na mwingine akajitokeza na kutishia kunipiga  risasi endapo ningeendelea kupiga kelele. Waliendelea  kunishambulia huku wakitaka niwape pesa “, alisema Kabengo  muda mfupi baada ya shambulio hilo wakati akisubiri matibu katika hospitali ya wilaya hiyo.
Majambazi hao walitokemea baada ya mke wa Kabengo kuwarushisa shilingi laki moja kupitia dirishani.
“ Nilimwambia mke wangu awape laki moja tuliyokuwa nayo ndani na majambazi walitaka awarushie kupitia dirishani”, alisema Mwalimu Kabengo huku akionesha kuhuzunishwa na tukio hilo la kinyama .
Polisi walifika nyumbani kwa mwalimu Kabengo mara baada ya tukio.
Juhudi za Mara Online News kumtafuta Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Tarime Rorya(RPC) Henry Mwaibambe kuzungumzia tukio hilo bado zinaendelea.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages