NEWS

Friday 23 August 2019

MILIONI 800 ZILIVYOHARAKISHA UJENZI WA HOSPITALI

           
           Na mwandishi wetu,
Hatimaye hospitali  ya Wilaya ya Serengeti imeanza kutoa huduma kwa wananchi  baada ya ujenzi wa baadhi ya majengo muhimu kukamilika.
Baadhi ya  huduma ambazo zimeanza kutolewa   katika hospitali hiyo  ni chanjo na  kiliniki  ya mama na mtoto.

Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mhandisi Juma Hamsini anasema hilo limewezekana  baada ya serikali ya awamu ya tano kuwapatia shilingi milioni 800.
Fedha hizo zimetumika kukamilisha na kuanzisha ujenzi wa baadhi  ya majengo  katika Hospitali hiyo ambyo inaelezwa   itakuwa ya kisasa baada ya ujenzi wake kukamilika .

   Hadi sasa tumepokea shilingi milioni 800 na zaidi ya shilingi milioni 680 zimetumika  kuboresha majengo yanayoonekana na kazi inaendelea “, Hamsini aliwaambia waandishi wa habari  ofisini kwake hivi karibuni .
    Tayari hospitali hii imeanza kutoa huduma kama vile chanjo, kliniki ya mama na mtoto   na ndani ya wiki moja kuanzia sasa wajazawazito wataanza kujifungulia  hapa”,  aliongeza Hamsini. 
Wananchi  wa mji wa Mugumu na vijiji jirani  wanaishukuru serikali ya awamu ya tano  kwa kutoa fedha  ambayo imesadia kuharakisha ujenzi wa hospitali  hiyo.

“ Napenda kumshukuru Mhe Rais John  Magufuli  kwa mchango wake ambao ametoa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali yetu ya Wilaya .Tunaomba mheshimiwa  Rais  aendelee kutuongezea  vitendea kazi ili watoto na wajawazito wasife “, anasema Mama Maiko ambaye ni mjasirimali katika soko la Mugumu .

DED Serengeti Mhandisi Juma Hamsini( wapli kulia) na Mwenyekiti wa kamati ya Ujenzi waHospitali ya Wilaya ya Serengeti  Charles Chacha ( wakwanza kushoto) wakikagua kazi inavyoendelea hivi karibuni.

Kutokana na kiu iliyokuwepo kwa  wananchi wa Serengeti kupata Hospitali ya wilaya , baadhi  ya wazee walijitolea kusimamia ujenzi  wa hospitali hiyo bila kuchoka .
“ Hospitali yetu hii itakapokamilika itakuwa ni fursa nzuri  sana kwa wakazi wa Serengeti  lakini pia itakuwa fursa  kwa watu wengine kutoka maeneo mbalimbali”,

Jambo la kufurahisha ni kwamba tayari ofisi za Mganga Mkuu wa Wilaya zimeanza rasmi kufanya kazi katika jengo la hospitali hiyo mpya ya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Ujenzi wa hosiptali  hiyo ulianza katika serikali ya awamu ya nne ambapo kwa kuanzia serikali ilitoa shilingi bilioni 1.6  kati ya mwaka 2009 na 2012 kwa ajili ya maandalizi ya awali.

Hamsini anasema fedha hizo zilitumika pamoja na mambo mengine  kusafisha eneo la ujenzi  kulipa fidia , kuweka mhandisi mshauri  na  kuanzisha ujenzi wa majengo ya  OPD( jengo kwa ajili ya wagongwa wa nje ).
Mwaka 2011 benki ya Afrika(AFD) ilifadhili ujenzi wa chumba cha upasuaji ( theater)na nyumba za watumishi  na baada ya hapo ujenzi wa hospitali hiyo ulisimama .

Mhandisi Juma Hamsini akionesha mashine ambayo itakuwa ikitumika kufua nguo katika hospitali ya Wilaya ya Serengeti
 SAFARI IKAANZA TENA 2016

Ujenzi wa hospitali hiyo ulisimama mwaka 2012 hadi  mwaka 2016 baada ya viongozi waliokuwa wameteuliwa na Rais John Magufuli kuanzisha kampeni ya jenga hospiliti kwa shilingi 1,000. Kampeni hiyo ilihusisha wananchi wa Serengeti na kisha kuungwa mkono na wadau wengine .

“ Tulianza na shilingi milioni 2.6  baadae wadau wakaanza kuonekana, watu wakachangia sementi, mchanga  SENAPA wakatoa milioni 50 , wenzetu wa WMA wakatoa milioni 100 na tukafanya kazi ikaonekana”,  anasema Mhandisi Hamsini.



 Baada ya kuonesha juhudi hizo, Mhandisi Hamasini anasema Rais Magufuli aliwapatia shilingi milioni 400 kusaidia ujenzi wa hospiatali hiyo.
“ Milioni 400 ndo imependezesha hayo majengo yanaonekena  yana rangi na umeme unawake lakini bado tulibaki na vifaa vingi”, anasema Mhandisi Hamsini.

Baada ya hapo Halmashauri hiyo pia ilipokea shilingi milioni 400 zingine ambazo zinaendelea kukamilisha na kuanzisha majengo mapya katika hospitali hiyo.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Serengeti kwa vipindi vitatu  tofouti John Ng’oina ambaye hivi sasa ni diwani wa kata ya Mbalibari  anasema  walianzisha ujenzi wa hospitali hiyo  kwa kuwa Wilaya hiyo ya Serengeti haijawahi  kuwa na hospitali ya Wilaya ya Serikali  jambo  lilikuwa ni tatizo kubwa kwa wananchi.



Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akimpongeza  aliyekuwa Mwenyekiti wa Hamashauri ya Wilaya ya Serengeti John Ngoin’a kwa vipindi vitano tofouti  kwa mchango wake katika  kunazisha ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Serengeti

Ng’oina   anasema jitahada za Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu  na wasaidizi wake pamoja na shilingi milioni 800 ambazo zimetolewa na serikali ya awamu ya tano zimeifikisha hosptalii hiyo mahali pazuri.
Jambo la kufurahisha ni kwamba  Halmashauri ya Serengti inagetemea pia kupokea shilingi milioni 500 katika mwaka huu wa fedha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa hospitali hiyo.
  Mwisho wa siku hospitali hii itakuwa ya kisasa na itakuwa ikitoa huduma bora kwa wananchi wa Serengeti”, anasema  Mhandisi Hamsini.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages