NEWS

Sunday 17 May 2020

PROF. SHEMDOE ATOA WITO KWA HALMASHAURI KUTENGA MAENEO YA UJENZI WA VIWANDA


Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Prof. Riziki Shemdoe ametoa wito kwa Halmashauri zote nchini kutenga maeneo maalumu ya uwekezaji kwa ajili ya ujenzi wa Viwanda katika mikoa yao.
Prof. Shemdoe aliyasema hayo Wilayani Kahama alipokuwa anakabidhiwa eneo la hekari 62 zilizotolewa bila fidia na Halmashauri ya mji ya Wilaya kahama kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa ajili ya kuanzisha kituo maalumu cha utafiti (centre of excellency) kitakachotumiwa na Taasisi za utafiti zilizo chini ya Wizara pamoja na taasisi nyingine kwa ajili ya utafiti unaolenga kuongeza thamani wa zao la pamba.
Prof. Shemdoe alisema “nimefarijika kuona namna halmashauri ya mji Kahama ilivyoweza kutekeleza agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda, kwa kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya uwekezaji.
“Nawashauri Halmashauri nyingine nchini kuja Kahama kujifunza jinsi Wilaya hii ilivyoweza kuendeleza maeneo hayo yaliotenga ikiwemo uwekaji wa miundombinu kama vile maji, umeme, bararabara na njia za mawasiliano”.
Prof. Shemdoe alisema eneo hilo walilokabidhiwa, kwa Wizara itajenga kituo kitakachotumika kuongeza thamani ya zao la Pamba.
“Tunatarajia kujenga kituo maalumu cha kutoa huduma za utafiti kwa zao la pamba ili mkulima aweze kufaidika na zao hilo kwa kuzingatia mnyororo wa thamani”.
Awali katika ziara hiyo, Prof. Shemdoe alitembelea eneo lilotolewa na Halmashauri kwa mwekezaji mzawa kampuni ya KOM group of Companies ambaye amejenga kiwanda kinachotarajiwa kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwemo maji, vinywaji na vifungashio.
Aidha, Prof. Shemdoe alitembelea eneo la Viwanda vidogo la Zongomela ambalo Halmashauri ya Wilaya Kahama imetoa kwa wajasiriamali wapatao 1500 wanaozalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo utengenezaji wa Samani, Mashine za kusagia mawe ya dhahabu na utengenezaji wa bidhaa za chuma na aluminiamu.
Naye Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack alieleza kuwa amefarijika kwa kuona Wizara imefika kuona kazi ambayo Halmashauri na Mkoa inafanya.
“Sisi kama Mkoa tulikaa chini na kuona namna ya kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais ya kuifanya Tanzania kuwa ya Viwanda, hivyo tukaamua kutekeleza kwa vitendo maagizo hayo”.
Aidha aliwashukuru Mamlaka ya Uendelezaji wa Mauzo ya nje EPZA kwa ushirikiano walioutoa kwa Halmashauri hiyo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages