NEWS

Wednesday 31 July 2019

AJALI YA HIACE YAUA 6 PAPO HAPO NA KUJERUHI 8 TARIME


       

Picha kutoka eneo la ajali




Na mwandishi wetu, Tarime 

 Watu sita wamekufa papo hapo leo mchana katika ajali ya gari ambayo imetokea  eneo la mteremiko  wa Nyamwaga jirani na mgodi wa North Mara Wilayani Tarime.
Aidha watu wengine 8 wamejeruhiwa vibaya katika ajali hiyo .

Jeshi la Polisi Mkoa wa Polisi  Tarime Rorya limetibithisha vifo sita  na majeruhi nane lakini inahofiwa kuwa idadi ya vifo inaweza kuwa zaidi ya sita
  Ajali  imehusisha gari la abiria aina hiace ambalo  lilikuwa linaelekea Mugumu Wilayani Serengeti.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema gari hilo lilipoteza uwelekeo na kutumbukia  kwenye korongo.

Tutaendelea  kukupatia taarifa zaidi kuhusu ajali hii.



1 comment:

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages