NEWS

Sunday 28 July 2019

CCM TARIME YATOA ONYO KWA WANAOMSEMA VIBAYA RAIS MAGUFULI


Kutoka kulia : Katibu wa CCM Wilaya ya Tarime Mkaruka Kura, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tarime Marwa Daudi Ngicho, Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Tarime Godfrey Francis na Katibu hamasa chipukizi Mkoa  wa Mara Mossy Magele.

 Na Clonel Mwegendao, Tarime

Uongozi wa chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Tarime umeapa kutofumbia macho viongozi wa upinzani wanaotukana viongozi wa serikali ya chama hicho na kupotosha wananchi kwa maneno ya uongo 

Akizungumza katika kikao cha baraza la kawaida la  UVCCM uliofanyika katika ukumbi wa ofisi za chama hicho wilaya Mwenyekiti a CCM  Wilaya ya Tarime  Marwa Daudi Ngicho amekemea vikali tabia ya baadhi ya viongozi wa upinzani kutoa maneno makali na yasiyokuwa ya kweli dhidi ya viongozi CCM nakuhaidi kuchukua hatua kali dhidi kiongozi yoyote atakayemchafua Rais Magufuli kwani kiongozi huyo ameweza kufanya maendeleo makubwa na yanaonekana.

Aidha amewataka vijana wote kufanya kazi kwa bidii katika kulinda na kutunza heshima ya CCM ikiwa ni pamoja na kumuenzi rais wa kwanza wa jamhuri ya muungano wa Tanzania hayati mwalimu Julius Kambarage Nyerere

“Fanya kazi kama mtumwa ili badae  uishi kama mfalme hivyo tufanye kazi kwa bidii ili tuondoe upinzani Tarime ili tuishi kwa amani na kuharakisha maendeleo yetu”alisema Ngicho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages