NEWS

Saturday 3 August 2019

WANAFUNZI WA NGOREME SEKONDARI WAPATA HOSTELI



Na Clonel Mwegendao

Wanafunzi wa shule ya sekondari Ngoreme iliyopo katika kata ya Kenyamonta wilayani Serengeti mkoani Mara wamekuwa wakitembea umbali wa takribani kilomita 12  kufika katika shule hiyo jambo ambalo limekuwa likipelekea  baadhi ya wanafunzi  kukosa masomo na kutopenda shule.

Akizungumza na Mara Online News leo kwa njia ya simu diwani wa kata ya Kenyamonta Sosteness Mwigicho Samwel amesema kuwa mpaka sasa kwa kushirikiana na wananchi pamoja na serikali wamefanikiwa kujenga hosteli ya kisasa kwa ajili ya wavulana na wasichana yenye uwezo wa kubeba wanafunzi 120 wakiwemo wavulana 80 na wasichana 40.


Hata hivyo ameweza kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano waliouonyesha katika kufanikisha ujenzi  wa hosteli hiyo na kutoa wito kwa jamii kuweka kipaumbele katika elimu ili kupata vijana wenye weledi jambo ambalo litasaidia kuwa na vijana wenye uwezo wa kuleta maendeleo katika jamii na taifa 











No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages