NEWS

Tuesday 3 September 2019

SIKU YA MARA DAY 2019: RC MALIMA ATAJA SHUGHULI MUHIMU ZITAKAZOFANYIKA


Mkoa wa Mara umepanga kupanda miti 100,000 katika Maadhimisho ya nane ya  siku ya Mara ambayo mwaka huu(2019) yatafanyika nchini Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Mara(RC) Adam Malima  amewaambia  waandishi wa habari ofisini kwake leo Septemba 03  kuwa  maadhimisho hayo yatafanyika  kuanzia Septemba 12-15  katika viwanja vya Sokoine mjini Mugumu, Wilayani Serengeti.

Mbali na shughuli za upandaji  miti,  RC Malima amesema kutakuwepo na maonesho ya bidhaa mbalimbali  yatakayohusisha wananchi na wadau wengine wa maendeleo .
 Mkuu huyo wa Mkoa amesema kauli mbiu ya Siku ya Mara Mwaka huu ni “ Mimi Mto Mara Nitunze Nikutunze”,

Aidha RC Malima  amesema Septemba 14 kutakuwepo na kongamano muhimu ambalo litahusisha  wadau wakubwa  wa bonde la mto Mara kutoka  Tanzania na Kenya.

Shughuli nyingine ambayo itakayofanyika katika maadhimisho hayo ni uwekaji wa lama za mipaka(beacons)  katika mipaka ya bonde la mto Mara na vijiji jirani.

 RC Malima amesema pia kutakuwepo na mashindano ya  michezo mbalimbali  katika maadhimisho
hayo. 
Mkuu wa Mkoa wa Mara akisisitiza umuhimu wa Maadhimisho ya siku ya Mara  katika mkutano wake na waandishi wa habari ofisini kwake

 Viongozi mbalimbali wa kitaifa kutoka mataifa hayo mawili wanatajaria kuhudhuria katika maadhimisho hayo ambayo kilele chake itakuwa ni Septemba 15 , amesema Mkuu wa Mkoa .
 Tanzania na Kenya huadhimisha siku ya Mara Septemba 15 kila mwaka kwa kupokezana ikiwa ni sehemu ya kuendeleza  juhudi za uhifadhi endelevu katika bonde la Mto Mara. 

Kwa kutambua umuhimu wa ikolojia ya Mara , kikao cha 10 cha Sekretarieti ya Mawaziri wa Bonde la Ziwa Victoria kilichofanyika Kigali nchini Rwanda  Mei 4,2012 kiliazimia Septemba 15  kila mwaka kuwa siku ya Mara .

 Maadhimisho ya  kwanza ya siku ya Mara  yalifanyika 2012  nchini Kenya na  kwa upande wa Tanzania maadhimisho ya kwanza ya siku ya Mara  yalifanyika 2013 .

TAZAMA VIDEO

           

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages