NEWS

Tuesday 17 September 2019

WIMBO WA MARA | SIKILIZA NA DOWNLOAD BURE



Kamisheni ya bonde la ziwa Victoria(LVBC) imezindua  wimbo wa Mara ambao  unahamsisha utunzaji wa  mazingira  ya  bonde la  Mara  kwa upande wa Kenya na Tanzania .
Katibu Mtendaji wa LVBC  Dkt Ali –Saidi Matano alizindua wimbo huo  Jumapili iliyopita  mara tu baada ya kilele cha maadhimisho ya nane ya siku ya Mara katika viwanja vya Sokine Mjini Mugumu Jana.
  “ Wimbo huu umekuja kwa wakati mwafaka na  tunaomba uimbwe kwenye redio, runinga, madukani na hata kwenye  mito wakati akina mama wanachota maji, na wafugaji wakati wakiwa kwenye malisho ya mifugo yao nan a wanafunzi mashuleni””,  Dkt Matano alisema.
Dkt Matano alishukuru shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira  na Wanyamapori(WWF) kwa kuja na wazo la kutumia njia ya wimbo katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mto Mara .
.Wimbo huo unamzungumzia  mama akiwa kwenye shida analia akihataji msaada na mama huyo ni mto Mara ,  alisema William Ojwang kutoka WWF Kenya .
“ Tunataka wimbo huu utumike kuendeleza kampeni ya kuhifadhi mto Mara na wimbo huu uendelee kutukumbusha kuwa mama yetu(mto Mara) analia na anahitaji msaada”,alisema Ojwang. 
         
   


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages