NEWS

Sunday 13 October 2019

KENYA WAADHIMISHA KUMBUKIZI YA MWALIMU NYERERE



Na mwandishi wetu, Nairobi 

Watanzania wanaoishi nchini Kenya , mabalozi wa  kutoka mataifa mbalimbali na  wananchi wa Kenya  jana Jumamosi Septemba 12, 2019  waliungana  na watanzania kuadhimisha kumbukizi  ya miaka 20 ya kifo  cha  Baba wa Taifa Tanzania  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere .


Balozi wa Tanzania nchini Kenya  Dr Pindi  Chana  aliongoza maadhimisho  hayo ambayo pia yalihudhuriwa  na mwanasheria maarufu wa Kenya  Profesa Patrice Lumumba.


Profesa Lumumba alisema Mwalimu Nyerere alikuwa nia mwaharakati na mkombozi wa kweli kwa baara la Afrika.

Aidha Profesa Lumumba alisema  Mwalimu Nyerere alikuwa ni moja ya viongozi waliaonzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Kwa upande wake Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dkt Chana  aliwashukuru wote  walioungana na  watanzania kuadhimisha  kumbukizi ya miaka 20 ya Mwalimu Nyerere.
 
 
Dr Chana alisema Mwalimu Nyerere ameendelea  kubaki kuwa ishara ya upendo sio tu kwa Tanzania bali kwa bara zima la Afrika.

“ Mwalimu alitufundisha, umoja, upendo, mshikamano na alitufundisha kuwa rushwa ni adui ya haki. Leo hii ni miaka 20 bila Mwalimu lakini kutokana na mawaidha na maneno yake  ni kama tupo naye hadi leo”, alisema Dr Chana.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages