NEWS

Tuesday 15 October 2019

MUSIBA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA



Na Raphael Okello, Bunda

VIJANA nchini  wametakiwa  kutumia fursa  zinazotolewa  na serikali
ya awamu  ya tano katika kubuni nafasi  za ajira  kwa kutumia vipaji
vyao badala ya kuendelea kulalamikia  nafasi za ajira.

Rai hiyo imetolewa jana  na Mwanaharakati  Huru  nchini, Cyprian
Musiba, alipokuwa  akikabidhi zawadi mbalimbali  kwa vijana  baada ya
mashindano  ya  Kombe la Magufuli(Magufuli Cup) yaliyofanyika  katika
viwanja vya  Kibara  jimbo la Mwibara wilayani Bunda mkoani  Mara.

Musiba  alisema kuwa Rais Magufuli katika awamu ya uongozi
anatekeleza miradi  mikubwa na midogo  kwa lengo la kutoa fursa kwa
vijana na kwamba ni juhudi  za vijana kutumia fursa hizo  kujikomboa
kiuchumi   na kuwataka vijana  kuchapakazi  na kuacha kujiingiza
katika  matumizi  ya madawa  ya kulevya.
 .

“Lengo la mashindano haya ya  ‘Magufuli Cup’ ni kupongeza na kuunga
mkono juhudi  hizi zote za Rais Magufuli  katika kuifikisha Tanzania
katika uchumi wa  kati.

Akizungumzia  siku  ya ukumbusho  ya kifo cha Baba wa Taifa  hayati
Mwalimu Julius Nyerere, Musiba alisema ,  Rais Dkt. Magufuli
anamuenzi  Baba wa taifa kwa kufanya yote aliyoanzisha  katika taifa
hili kipindi cha uhai wake jambo ambalo hakuna Mtanzania  mwenye nia
njema na nchi yake anayeweza kupinga.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages