NEWS

Friday 11 October 2019

NAMBA 3 ATUNUKIWA CHETI KWA MCHANGO WAKE KATIKA MAENDELEO YA JAMII




Na Amina Kakiva,
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara Samwel Kiboye Namba Tatu jana  ametunukiwa cheti na taasisi ya Professor Mwera Education Foundation kwa kutambua mchango wake anaoutoa katika maendeleo ya  jamii .
Mwenyekiti huyo alikuwa mgeni rasmi katika  mahafali ya pili ya kidato cha nne katika shule ya sekondari ya  wasichana  ya Tarime.
Katika hotuba yake  Namba tatu aliwaonya vikali vijana wanaoendesha bodada kuacha kuwarubuni wanafunzi  wa kike  jambo ambalo linakatisha ndoto zao kielimu.
Aidha Mwenyekiti huyo wa CCM  alitoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Mara kuwapatia fursa watoto wa kike kusoma baadala ya kuwaozesha mapema kwa lengo la kupata  mahari .
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Professor Mwera Education Foundation Peter Mwera alisema uwekezaji katika elimu ya vijana ni jambo linalopaswa kupewa umuhimu mkubwa.
Jumla ya wanafunzi wa kike 44 walitunukiwa vyeti vya kihitimu elimu katika mahafali hayo. 




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages