NEWS

Wednesday 15 April 2020

Bariadi watakiwa kutochangia chombo cha kunawia mikono



Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Festo Kiswaga amewataka wananchi wilayani humo kuacha tabia ya kunawa mikono kwenye chombo kimoja kama vile bakuli na beseni, badala yake watumie maji yanayotiririka kuepuka maambukizi ya corona (COVID-19).
   “Tusitumie bakuli moja kunawa mikono kwa kuitumbikiza ndani, badala yake tumie maji yanayotiririka. Ndani ya familia, hususan wakati wa kula ni vema kila mmoja anawe maji yake hata kwa kumwagiliziana,” amesisitiza Kiswaga.
   Aidha, Kiswaga amepiga marufuku michezo yote na sherehe zinazofanyika katika mikusanyiko na kuwahimiza wananchi wote kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na serikali katika kuchukua tahadhari dhidi ya janga hilo la kimataifa.
   “Jikinge na corona, zingatia ushauri wa wataalamu wa afya, afya yako, mtaji wako. Bariadi bila maambukizi ya corona inawezekana,” amasema Kiswaga.

(Habari na Anita Balingilaki, Bariadi)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages