NEWS

Friday, 6 June 2025

TAMISEMI yatoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano, vyuo vya kati 2025


Wakati Serikali ikiendelea na juhudi za kuboresha elimu nchini, imetangazwa rasmi kuwa jumla ya wanafunzi 214,141 wakiwemo wasichana 97,517 na wavulana 116,624 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Elimu ya Ufundi kwa mwaka wa masomo 2025, baada ya kukamilika kwa mchakato wa uchaguzi wa wanafunzi uliozingatia Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 (toleo la 2023) pamoja na mtaala ulioboreshwa.

Taarifa hiyo imetolewa kwa waandishi wa habari na Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati wa mkutano uliofanyika jijini Dodoma, ambako viongozi kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI na wadau wa elimu walikutana kutangaza rasmi matokeo ya uchaguzi huo muhimu kwa mustakabali wa elimu nchini.

Waziri Mchengerwa ameleza kuwa kati ya wanafunzi waliochaguliwa, 149,818 wamepangwa katika shule za sekondari za Serikali zipatazo 694, ambapo wanafunzi 1,728 walipangwa katika shule nane (8) zenye ufaulu wa juu zaidi, 141,146 katika shule za bweni, na 6,944 katika shule za kutwa.
Read Also Section Example

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages