NEWS

Sunday 26 April 2020

Mwanza wakaidi bei elekezi ya sukari


WAFANYABIASHARA wengi jijini Mwanza wameendelea kuuza sukari kwa bei ya juu licha ya serikali kutangaza bei elekezi ambayo ni kati ya Sh 2,600 na 3,000 nchini.

Uchunguzi uliofanywa na Mara Online News leo Jumapili Aprili 26, 2020 katika baadhi ya mitaa ikiwamo Uhuru, Liberty na Mitimirefu jijini hapa, umebaini uwepo wa maduka yanayouza sukari kati ya Sh 3,200 na 3,500.

Hivi karibuni Serikali ya kupitia kwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa, ilitangaza bei elekezi ili kudhibiti upandaji holela wa bei ya sukari nchini.

Kwa mujibu wa Sheria ya Sukari Namba 20 ya Mwaka 2001 (kifungu cha 251) chini ya kifungu cha 11A, waziri mwenye dhamana ya viwanda na biashara ana mamlaka ya kutangaza bei ya kikomo ya bidhaa hiyo.

(Habari na Suleiman Shagata, Mwanza)





No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages