NEWS

Thursday 18 June 2020

DC abaini tegesha mpya Nyamongo, wathamini, mwenyekiti matatani


MKUU wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Mhandisi Mtemi Msafiri, jana Juni 18, 2020 amesemea hatasaini kupitisha malipo kwa ajili ya wananchi wa kijiji cha Komarera waliotegesha mazao na miti  kwa lengo la kulipwa fidia kutoka Mgodi wa Dhahabu wa North Mara uliopo Nyamongo.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri (mwenye fimbo) akikagua mazao yaliyotegeshwa katika kijiji cha Komarera


Mhandisi Msafiri ametoa msimamo huo alipotembelea eneo ambalo limefanyiwa tathimini na kushuhudia mazao yaliyotegeshwa katika eneo hilo ndani ya muda mfupi baada ya wananchi kubaini kuwa eneo hilo linahitajika kwa upanuzu wa shughuli za mgodi huo.

Aidha, mkuu huyo wa wilaya ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuwahoji wathamini waliohusika kutathimini vitu vilivyotegeshwa katika eneo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri akionesha zao lililotegeshwa katika kijiji cha Komarera

Pia ameagiza Jeshi la Polisi wilayani Tarime kumtia nguvuni Mwenyekit wa Serikali ya Kijiji cha Komarera, Nyamganya Marwa, kwa anayetuhumiwa kuhamasisha wananchi kutegesha mazao na miti katika eneo hilo.

Uthamini katika eneo hilo umefanywa hivi karibuni na Kampuni ya Whiteknights Real Estates Investment Co. Ltd.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages