NEWS

Friday 12 June 2020

Nyanswi Mwenyekiti mpya CHADEMA Tarime


Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimejaza nafasi iliyokuwa wazi ya mwenyekiti wa wilaya ya Tarime kwa kumchagua Mwenyekiti wa Halmashauri yaTarime Hamis Nyanswi kuwa mwenyekiti mpya wa CHADEMA katika  wilaya hiyo yenye  majimbo mawili ya Tarime Mjini na Tarime vijijini.
Nyanswi(pichani anayeongea kushoto) amepata uhsindi wa kishindo kushika nafasi  hiyo katika uchaguzi uliofanyika leo 12 Juni 2020 katika ofisi ya wilaya ya chama hicho mjini Tarime.

Akitangaza matokeo msimamizi wa uchaguzi huo Mahonia Joseph amemtangaza Nyanswi  kuwa mshindi baada ya kupata kura 18 kati 19 zilizopigwa .
Mshindani wake Jacob Kayelle ameambulia kura moja.

" Na Clonel Mwegendao, Tarime)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages