Madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Tarime, Mkoani Mara leo Machi 1,2021 wameanza kupata mafunzo yanayolenga kuwawezesha kutekeleza wajibu wao kwa ufanisi.
Mafunzo
hayo yatahusisha mada 18
zikiwemo, uongozi na utawala bora, sheria za uendeshaji wa Serikali za mitaa,
muundo, madaraka na majukumu ya Serikali za mitaa, maadili
ya utumishi wa umma, uibuaji na utekelezaji wa miradi ya kijamii.
Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Tarime wakishiriki katika mafunzo hayo |
“Naipongeza sana Halmashauri ya Mji Tarime kwa kuona
umuhimu wa kuendesha mafunzo haya kwa madiwani. Hii ni Shule tosha na baada ya mafunzo hayo Halmashauri na iwe
bora na yenye kasi kubwa ya kuwaletea wananchi wetu maendeleo’, DAS Marwa
ambaye amefungua mafunzo hayo kwa niaba
ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime (DC) Mhandisi Mtemi Msafiri amesema.
“ Lengo ni kuwajengea uwezo madiwani wetu kuna mada 18 katika mafunzo haya na
yanahusisha pia Wabunge wetu “, amesema
Ntiruhungwa .
Mkurugenzi wa Mji wa Tarime, Elias Ntiruhungwa akitoa maelezo kuhusu mafunzo hayo. |
“ Mafunzo hayo yana faida kubwa kwa Halmashauri yetu na wananchi wetu”, amesema Komote ambaye ni diwani wa kata ya Nkende kupitia chama tawala (CCM).
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Tarime, Daniel
Komote akisisitiza umuhimu wa mafunzo
hayo
CCM ilishinda viti vyote vya udiwani katika jimbo la Tarime katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka jana.
No comments:
Post a Comment