NEWS

Tuesday 14 September 2021

DC Tarime Azindua Maadhimisho ya Kumi ya Mara Day

MGENI Rasmi katika Uzinduzi wa Maadhimisho ya Kumi ya Siku ya Mara, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Col. Michael Mntenjele(aliyevaa kofia), akimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha Bodi ya Maji ya Bonde la Ziwa Victoria, Perpetua Masaga.

MKUU wa Wilaya ya Tarime, Col. Michael Mntenjele leo amezindua rasmi Maadhimisho ya 10  ya Siku ya Mara ambayo yanatarajiwa kufikia kilele Kesho.

Uzinduzi huo umefanyika kwenye viwanja vya Chuo cha Ualimu Tarime, baada ya DC huyo kutembelea mabanda ya mamlaka, taasisi na mashirika mbalimbali ya serikali na binafsi kwenye viwanja hivyo.

Mapema leo asubuhi , DC Mntenjele aliongoza viongozi na wadau wa mazingira kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Mara, kupanda miti kando ya Mto Mara katika Vijiji vya Mrito na Kerende.

Amesema jumla ya miti 15,000 imepandwa tangu juzi, jana na leo pamoja na Bicon (Vigingi) 70 zimesimikwa ikiwa sehemu ya shughuli za maadhimisho hayo kwa Mwaka huu. Mgeni rasmi katika  kilele cha maadhimisho hayo anatarajiwa kuw  Waziri wa Maji, Jumaa Aweso.

Maadhimisho ya kwanza ya Siku ya Mara yalifanyika mwaka 2012 nchini Kenya na kwa upande wa Tanzania yalifanyika mwaka 2013 katika mji wa Mugumu, wilayani Serengeti.

Kaulimbiu ya maadhimisho hayo mwaka huu ni: "Tuhifadhi Mto Mara kwa Utalii na Uchumi Endelevu",

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages