NEWS

Monday, 17 November 2025

Rais Samia atangaza baraza jipya la mawaziri, apumzisha vigogo saba



Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akitangaza baraza jipya la mawaziri Ikulu Chamwino jijini Dodoma, leo Jumatatu Novemba 17, 2025.

Na Mwandishi Wetu
Dodoma
------------

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza baraza jipya la mawaziri 27, ikiwa ni sehemu ya kurekebisha utendaji na kuongeza ufanisi ndani ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo Jumatatu Novemba 17, 2025, Rais Samia amesema mabadiliko hayo yanahusisha kuanzishwa kwa wizara mpya, kubadilishwa kwa baadhi ya wizara za zamani na kuingizwa kwa sura mpya serikalini.

Miongoni mwa walioteuliwa kwa mara ya kwanza ni Dkt. Rhimo Nyansaho ambaye amepewa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, na Joel Nanauka aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Wizara mpya Maendeleo ya Vijana itakayokuwa chini ya Ofisi ya Rais.

Rais Samia pia amewarejesha mawaziri kadhaa waliokuwa serikalini, akiwemo Prof. Adolph Mkenda, Jumaa Aweso, Prof. Makame Mbarawa na Profesa Paramagamba Kabudi.

Hata hivyo, baadhi ya mawaziri maarufu kama Hussein Bashe aliyekuwa akiongoza Wizara ya Kilimo, hawakurejea katika baraza jipya.

Pia, Dotto Biteko aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ameachwa kama ilivyo kwa Waziri wa muda mrefu, Jenista Mhagama (Afya) na Damas Ndumbaro (Katiba na Sheria).

Wengine waliotemwa ni Suleiman Jaffo (Viwanda na Biashara), Innocent Bashungwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Pindi Chana (Maliasili na Utalii).

Katika mabadiliko hayo, Rais Samia ametangaza kuanzishwa kwa Wizara ya Maendeleo ya Vijana chini ya Ofisi ya Rais, huku Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana ikibadilishwa kuwa Wizara ya Kazi, Ajira na Mahusiano, ambayo sasa itakuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

Aidha, Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ambayo kwa miaka mingi imekuwa chini ya Ofisi ya Rais, sasa imehamishiwa rasmi Ofisi ya Waziri Mkuu.

Ifuatayo ndiyo orodha kamili ya Mawaziri na Naibu Mawaziri walioteuliwa:

1. Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waziri: Ridhiwani Jakaya Kikwete

Naibu Waziri: Regina Ndege Qwaray

2. Ofisi ya Rais – Mipango na Uwekezaji

Waziri: Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Naibu Waziri: Pius Stephen Chaya

3. Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana- Waziri: Joel Arthur Nanauka

4. Ofisi ya Makamu wa Rais – Muungano na Mazingira

Waziri: Mhandisi Hamad Yusuf Masauni

Naibu Waziri: Dkt. Festo John Dugange

5. Ofisi ya Waziri Mkuu – Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu

Waziri: William Vangimembe Lukuvi

Naibu Waziri: Ummy Hamisi Nderiananga

6. Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano

Waziri: Deus Clement Sangu

Naibu Waziri: Rahma Riadh Kisuo

7. Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)

Waziri: Prof. Riziki Silas Shemdoe

Naibu Waziri (Elimu): Reuben Nhamanilo Kwagilwa

Naibu Waziri (Afya): Jafar Rajab Seif

8. Wizara ya Fedha

Waziri:Balozi Khamis Mussa Omar

Naibu Waziri: Laurent Deogratius Luswetula

Naibu Waziri: Mshamu Ali Munde

9. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Waziri: Balozi Mahmoud Thabit Kombo

Naibu Waziri: Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe

Naibu Waziri: James Kinyasi Millya

10. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Waziri: Boniface George Simbachawene

Naibu Waziri: Denis Lazaro Londo

11. Wizara ya Kilimo

Waziri: Mhe. Daniel Godfrey Chongolo

Naibu Waziri: Mhe. David Ernest Silinde

12. Wizara ya Maji

Waziri: Jumaa Hamidu Aweso

Naibu Waziri: Kundo Andrea Mathew

13. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa-Waziri: Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho

14. Wizara ya Ujenzi

Waziri: Abdallah Hamis Ulega

Naibu Waziri: Mhandisi Godfrey Msongwe Kasekenya

15. Wizara ya Uchukuzi

Wazir:Prof. Makame Mbarawa Mnyaa

Naibu Waziri: David Mwakiposa Kihenzile

16. Wizara ya Viwanda na Biashara

Waziri: Judith Salvio Kapinga

Naibu Waziri: Patrobas Paschal Katambi

17. Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Waziri: Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Naibu Waziri: Switbert Zacharia Mkama

18. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum

Waziri: Dkt. Dorothy Onesphoro Gwajima

Naibu Waziri: Maryprisca Winfried Mahundi

19. Wizara ya Afya

Waziri: Mohamed Omary Mchengerwa

Naibu Waziri: Dkt. Florence George Samizi

20. Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Waziri: Prof. Adolf Faustine Mkenda

Naibu Waziri:Wanu Hafidh Ameir

21. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Waziri: Leonard Douglas Akwilapo

Naibu Waziri:Kaspar Kaspar Mmuya

22. Wizara ya Maliasili na Utalii

Waziri: Mhe. Ashatu Kachwamba Kijaji

Naibu Waziri: Hamad Hassan Chande

23. Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo

Waziri: Prof. Palamagamba John Kabudi

Naibu Waziri: Hamisi Mwinjuma

Naibu Waziri:Paul Christian Makonda

24. Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Waziri: Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa

Naibu Waziri: Mhe. Ng’wasi Damas Kamani

25. Wizara ya Madini

Waziri: Anthony Peter Mavunde

Naibu Waziri: Dkt. Steven Lemomo Kiruswa

26. Wizara ya Nishati

Waziri: Deogratius John Ndejembi

Naibu Waziri: Salome Wycliffe Makamba

27. Wizara ya Katiba na Sheria

Waziri: Juma Zuberi Homera

Naibu Waziri: Zainabu Athman Katimba

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages