NEWS

Wednesday 17 January 2024

Rais Samia azindua Tawi la CCM Chaani Masingini visiwani Zanzibar




RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt Samia Suluhu Hassan (pichani katikati), leo Januari 17,2024 amezindua ofisi ya Chama hicho Tawi la Chaani Masingini lililopo mkoa wa Kaskazini Unguja wakati wa ziara yake ya kikazi visiwani Zanzibar.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais Dkt Samia ametoa wito kwa wanachama wa CCM kujiandaa na chaguzi zijazo, lakini pia kudumisha umoja na mshikamano.

Ujenzi Wa ofisi hiyo umegharimu shilingi milioni 248, ambapo ndani yake kuna ofisi za jumuiya zote za CCM.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages