NEWS

Monday, 15 July 2024

Hispania yashinda Euro tena kwa mara ya nne



Kikosi cha timu ya Hispania wakifurahia ushindi wao wa Euro 2024 baada ya Kuinyuka Uingereza 2-1
                              -------------
Hispania ilishinda michezo yote saba bila kuhitaji mikwaju ya penati, rekodi mpya katika Mashindano ya Ulaya. Ushindi wa 2-1 dhidi ya Uingereza katika fainali uliwafanya kuwa mabingwa wa Ulaya kwa mara ya nne.

Walipata ushindi kwa njia ngumu, wakishinda mataifa mengine yote ya Ulaya ambayo yamewahi kushinda Kombe la Dunia - Italia, Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, pamoja na Croatia waliofika fainali mwaka 2018 - kuelekea ushindi wao huko Berlin.

Rodri alikuwa mchezaji bora wa mashindano. Lamine Yamal alikuwa mchezaji mdogo bora. Dan Olmo alishinda tuzo ya kiatu cha dhahabu ‘Golden Boot’. Yamal alikuwa na msaada mkubwa katika kupatikana kwa magoli ya timu yake ya Taifa kwa maana ya kutoa ‘assist’ nyingi

Ni rahisi kusahau kuwa hawakuingia katika mashindano kama Kipenzi cha mashabiki wengi, ambapo Uingereza na Ufaransa walikuwa wanatarajiwa kuibuka washindi.

Hata kocha wa Uingereza, Gareth Southgate, alikubali kwamba Hispania walistahili kuwa mabingwa.

"Hongera Hispania. Walistahili kushinda sio tu usiku huu, bali katika mashindano yote," aliongeza kocha wa Uingereza

CHANZO: BBC NEWS

UNAWEZA PIA KUSOMA:

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages