
Meneja Mahusiano wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Francis Uhadi (katikati aliyevaa jaketi ya njano) na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mara, Mary Daniel Joseph (kulia kwa Uhadi), wakifurahia picha ya pamoja na vijana waliofanya ziara ya mafunzo mgodini hapo Jumatano iliyopita.
----------------------------------
Na Mwandishi Wetu, Tarime
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Mara, Mary Daniel Joseph, ameongoza viongozi wa makundi mbalimbali ya vijana kutembelea Mgodi wa Dhahabu wa North Mara, unaoendeshwa kwa ubia kati ya kampuni ya Barrick na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni Twiga Minerals.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Mara, Mary Daniel Joseph akizungumza wakati wa ziara yao ya mafunzo mgodini hapo.
----------------------------------
Katika ziara hiyo, vijana hao walipata fursa ya kuelewa kwa undani namna Mgodi wa North Mara unavyofanya shughuli zake na kutekeleza miradi ya Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR), jinsi unavyowawezesha vijana wa maeneo Jirani kiuchumi, hatua za usalama kazini, pamoja na mbinu za kisasa za uhifadhi wa maji taka na maji safi.
Mwenyekiti Mary alitumia nafasi hiyo pia kuwahimiza vijana walioshiriki ziara hiyo kuwa mabalozi wema kwa jamii zao kuhusu umuhimu na faida za uwekezaji wa mgodi huo wa Barrick North Mara.
“Nendeni mkawe mabalozi wema kwenye jamii zenu, waelezeni wananchi kwamba mgodi wa North Mara ni watu wanaofikika, ni rafiki kwa jamii, wasaidieni kutatua changamoto zilizopo,” Mary alisema Kwa msisitizo.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
»Ajali yakatisha maisha ya Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji Tarime
»MAKALA:Ushirika wa WAMACU wamshukuru Rais Samia uzinduzi wa Benki ya Ushirika Tanzania
»Meja Gowele awa Mkuu wa Wilaya wa kwanza kutangaza Mlima Tarime kivutio cha utalii
»Elizabeth Msabi arejea kutoka UK, awa mwanamke wa kwanza kutangaza nia ya ubunge Tarime Vijijini kupitia CCM
No comments:
Post a Comment