NEWS

Monday, 16 June 2025

Wahitimu wa zamani Sekondari ya Mogabiri warudisha shukrani kwa msaada wa kompyuta 11




Na Godfrey Marwa, Tarime

Umoja wa Wahitimu wa Zamani Shule ya Sekondari Mogabiri iliyopo Halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara umeipatia shule hiyo msaada wa kompyuta 10 na kompyuta mpakato moja ili kuinua kiwango cha taaluma kwa wanafunzi.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, mwakilishi wa Mwenyekiti wa Umoja huo, Tumaini Jonathan Mwambara, alisema wamechukua hatua hiyo kurudisha shukrani zao shuleni hapo.

"Tumeona ni vyema kurudisha kidogo kwa shule iliyotufanikisha. Msaada huu utasaidia kuinua kiwango cha elimu ya TEHAMA, kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kidijitali, kuwaandaa vyema katika soko la ajira na dunia ya sasa yenye ushindani mkubwa.

“Tunaahidi kuendelea kushirikiana na shule hii, na tunatoa wito kwa wahitimu wengine kujitokeza kushiriki katika juhudi hizi za maendeleo," alisema Mwambara.
Afisa Elimu kata ya Ketare, Bestina Subi, alishukuru akisema: "Niwashukuru sana wanafunzi waliowahi kusoma hapa - wamekumbuka nyumbani, msiishie hapo. Wanafunzi mnahitaji kusoma kwa bidii."

Naye Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Magudira Mugeta, aliushukuru umoja huo na kuuomba kuendelea na moyo huo wa upendo na kujitolea.

"Nawashukruni sana, msichoke kusaidia tena kwa sababu manufaa mliyonayo mmeyapata hapa Mogabiri Sekondari. Nawakaribisha mje mara nyingine ili Mogabiri yetu tuendelee kuiinua," alisema.

Nao wanafunzi wa shule hiyo walishukuru na kuahidi kusoma kwa bidii, na kutunza vifaa hivyo kwa manufaa yao na watakaofuata.


Read Also Section Example

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages