NEWS

Monday 22 July 2019

AJALI YAUA 4 NA KUJERUHI 15 KAHAMA



























Na mwandishi wetu

Watu 4 wamefariki dunia na wengine 15 kujeruhiwa   katika ajali ambayo imehusisha magari mawili aina ya Toyota Hiace na LandCruiser   katika Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga  .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga(RPC) Richard Abwao amesema ajali hiyo   ilitokea  jana usiku Julai 21 katika eneo la Nyambula kata ya Ngogwa.

“ Waliokufa ni 4 wakiwemo watoto watatu na mtu mzima mmoja  na majeruhi ni 15 ambao wanapata matibabu katika hospitali ya Kahama”, RPC Abwao ameiambia Mara Online News kwa njia ya simu leo asubuhi.

 RPC Abwao amesema hali za majeruhi zinaendelea vizuri.
“ Tunawashikiria pia madereva wote wawili ambao pia ni majeruhi na wapo hospitali”, aliongeza


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages