NEWS

Sunday 21 July 2019

RAIS MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MAKAMBA | +VIDEO

Mbunge wa Bumbuli (CCM) January  Makamba

                                 
 Na mwandishii wetu
Rais John Magufuli leo Julai 21 ametengua uteuzi wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa  Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba na kumteu George  Simbachawene kuchukua nafasi yake.
Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa ambayo imetolea kwa vyombo vya habari leo asubuhi imesema Rais Mgufuli pia amemteua Hussein Bashe kuwa Naibu Waziri wa Kilimo kuchukua  nafasi ya Innocent Bashungwa ambaye aliteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara hivi karibuni.
Rais Magufuli pia amemteua Balozi Martin Lumbanga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibithi wa Ununuzi wa Umma(PPRA) kushika nafasi hiyo kwa kipindi cha pili.
“ Uteuzi wa viongozi hao  unaanza leo tarehe 21 Julai,2019”, imesema taarifa hiyo.





No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages