NEWS

Monday 23 September 2019

WADAU WAKUTANA KUJADILI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA



Wadau wa uchaguzi wa serikali za mitaa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime wamekutana leo Septemba 23, 2019  kujadili taratibu na kanuni za uchaguzi utakaofanyika Novemba 24 mwaka huu.




Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Jane Tungu amesema kuwa uchaguzi utafanyika kuanzia saa mbili  kamili asubuhi hadi  saa kumi na mbili jioni katika majengo ya umma na mitaa  isiyo na majengo  ya umma watapendekeza  sehemu ambayo itakuwa rafiki kwa uchaguzi huo.



Miongoni mambo yaliyojadiliwa katika mkutano huo wa wadau uliofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari ya Tarime ni uraia ,umri,utimamu wa akili na kutokuwa na kumbukumbu za uhalifu.



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages