NEWS

Saturday 25 January 2020

DC SERENGETI AKABIDHI MIPANGO YA MATUMIZI BORA KWA VIJIJI 8



Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu jana Januari 24 alikabidhi vitabu vya mipango ya matumzi bora ya ardhi kwa viongozi wa vijiji 8 na kuwataka viongozi hao kutekeleza mipango hiyo kikamilifu ili kuondoa migogoro ya ardhi pamoja migogoro kati ya wanyamapori na binadamu.

 Babu pia alikabidhi kitabu chenye mpango wa matumizi bora ya ardhi wa miaka 20  wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Juma Porini.
  

Zoezi la kuandaa mipango hiyo umefadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Ujerumani(KfW) na kuwezeshwa na  Shirika la Frankfurt Zoological Society(FZS) kwa kushirikiana na  Shirika la Hifadhi za Taifa(TANAPA).

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages