NEWS

Monday 20 July 2020

TASAF yawezesha mafunzo ya uhakiki walengwa Tarime Mji


Mkurugenzi  wa Halmashauri ya Mji wa Tarime Elias Ntiruhungwa  akiongea na wakuu wa idara pamoja na wawezeshaji katika mafunzo ya uhakiki wa kaya maskini yaliyoandaliwa na TASAF
Mafunzo hayo ya siku mbili ambayo pia yamehusisha wakuu wa idara wa Halmshauri hiyo yatafuatiwa na kazi ya uhakiki wa kaya za walengwa kwa lengo la kuondoa wanufaika hewa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tarime, Elias Ntiruhungwa, amewataka washiriki wa mafunzo hayo kufanikisha kazi hiyo inayotarajiwa kufanyika kote nchini.


Kwa upande wake, Nisalile Brown Mwaipasi(anayeongea pichani) kutoka TASAF, amesema kazi ya uhakiki inalenga kusafisha daftari la walengwa.
 Mwaipasi amesema takwimu zinaonesha kuwa utekelezaji wa mpango huo kwa kipindi cha kwanza umechangia kupunguza umaskini wa mahitaji ya msingi kwa kaya kwa asilimia 10 na umaskini uliokithiri umepungua kwa asilimia 12 kwa kaya maskini sana nchini.
 
Wakuu wa idara na wawezeshaji  wa TASAF  katika Halmashauri ya Mji wa Tarime wakiwa kwenye mafunzo leo
 (Imeandikwa na Mara Online News, Tarime

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages