NEWS

Monday 21 June 2021

PICHA YA SIKU – (Dkt Mashinji na Nassari wanapokutana tena kwa mlango mwingine)



OOH tumekutana tena, sasa tuchape kazi za maendeleo. Ndivyo wanavyoonekana kuteta wanasiasa hao wawili; Dkt Vicent Mashinji (wa pili kushoto) ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani - CHADEMA kabla kuhamia chama tawala - CCM na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kwa tiketi ya CHADEMA, Johua Nassari (wa pili kulia), wakati wa hafla ya kuapishwa kushika wadhifa wa ukuu wa wilaya, iliyofanyika mjini Musoma leo Jumatatu Juni 21, 2021, ambapo Nassari sasa ni Mkuu mpya wa Wilaya ya Bunda na Dkt Mashinji ni Mkuu mpya wa Wilaya ya Serengeti. Wa kwanza kushoto ni Mkuu mpya wa Wilaya ya Rorya mkoani Rorya, Juma Issa Chikoka.

MaraOnlineNews-Updates

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages