Mto Mara ni sehemu muhimu ya ikolojia ya Serengeti, kwani una mchango mkubwa katika uhifadhi wa wanyamapori, wakiwemo nyumbu ambao ni kivutio kikubwa cha utalii kutokana na matukio yao ya kipekee, hususan ya kuvuka mto huo kwenda Mbuga ya Maasai-Mara, kisha kurudi Serengeti kila mwaka.
Mto huo unaanzia kwenye chemichemi za Enopuyapui katika misitu ya Mau nchini Kenya, kisha kupita Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kumwaga maji yake katika Ziwa Victoria, upande wa Tanzania.
Mto huo unaanzia kwenye chemichemi za Enopuyapui katika misitu ya Mau nchini Kenya, kisha kupita Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kumwaga maji yake katika Ziwa Victoria, upande wa Tanzania.
Mbali na uhifadhi wa ikolojia ya Serengeti, Bonde la Mto Mara lina mchango mkubwa katika ustawi wa maisha ya watu zaidi ya milioni 1.1 katika nchi za Tanzania na Kenya.
Aidha, Mto Mara ni muhimu kwa shughuli mbalimbali za binadamu, zikiwemo za kilimo cha umwagiliaji, maji kwa ajili matumizi ya nyumbani, mifugo na uvuvi. Lakini pia, mto huo unachangia kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Kenya, kupitia maadhimisho ya Siku ya Mara, inayoadhimishwa Septemba 15 kila mwaka.
Eneo la Bonde la Mto Mara lina ukubwa wa kilomita za mraba 13,325, huku mto wenyewe ukiwa na urefu wa kilomita 400.
MaraOnlineNews-Updates
Aidha, Mto Mara ni muhimu kwa shughuli mbalimbali za binadamu, zikiwemo za kilimo cha umwagiliaji, maji kwa ajili matumizi ya nyumbani, mifugo na uvuvi. Lakini pia, mto huo unachangia kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Kenya, kupitia maadhimisho ya Siku ya Mara, inayoadhimishwa Septemba 15 kila mwaka.
Eneo la Bonde la Mto Mara lina ukubwa wa kilomita za mraba 13,325, huku mto wenyewe ukiwa na urefu wa kilomita 400.
MaraOnlineNews-Updates
No comments:
Post a Comment