NEWS

Friday 6 August 2021

KADA WA CHADEMA APATA CHANJO YA UVIKO -19 TARIME

KADA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Mara, Mwalimu Chacha Heche ameshiriki kupokea chanjo ya UVIKO-19 na kuwahimiza wafuasi wa chama hicho kujitokeza.

Mwalimu Heche ambaye ni kiongozi wa Mafunzo Chadema makao makuu amesema kuwa amejitokeza baada ya kushauriana na madaktari wake wakamhakikishia kwamba chanjo hiyo ni salama hivyo ameitaka serikali itoe elimu kwa jamii.

“Niko hapa kwa ajili ya kupata chanjo ya korona, kimsingi nimefanya mawasiliano kwanza na madaktari wangu, watu wa afya wakanishauri kwamba ni muhimu nikapata hiyo chanjo, kwangu mimi chanjo sio kitu kigeni nimewahi kupokea chanjo ya homa ya ini na zingine”, amesema Heche.


Heche ambaye amewahi kuwa mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Mara, amewashauri wafuasi wa chama hicho kushiriki kupokea chanjo bila kujali utofauti za kiitikadi zilizopo kati yao na serikali kwani afya ni jambo la msingi.

“Pamoja na tofauti yangu ya kiitikadi na serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu, kwamba mimi ni kiongozi wa mafunzo Chadema, lakini kwenye masuala ya msingi kama suala la afya hutakiwi kuleta tofauti ambazo zinaweza kupotosha watu na kuwachanganya, kwa sababu unamitazamo tofauti na serikali”, amesema Heche baada ya kupokea chanjo hiyo.   

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages