NEWS

Monday 20 May 2024

MNEC Joyce Mang’o ashinda Tuzo ya Mwanamke wa Shoka 2024


MNEC Joyce Ryoba Mang'o akionesha Tuzo aliyoshinda ya Mwanamke wa Shoka mwenye Uthubutu kwa Mwaka 2024.
------------------------------------------------

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
----------------------------------------


Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Mkurugenzi wa Joma Ubunifu, Joyce Ryoba Mang'o ametunukiwa Tuzo ya Mwanamke wa Shoka mwenye Uthubutu kwa Mwaka 2024.

MNEC Joyce alikabidhiwa tuzo hiyo juzi katika ukumbi wa Mabeyo Hall jijini Dodoma, baada ya kuonekana ana mchango mkubwa na uthubutu katika jamii.

Tuzo hiyo iliandaliwa na EFM, KITCHEN GALLA 2024 NA DINA MARIUS ambaye pia amekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha na kuhakikisha wanawake wanakuwa na uthubutu wa hali ya juu.

Hiyo ni tuzo ya pili kwa MNEC Joyce kwa mwaka huu kwani alishinda Tuzo ya Ujasiriamali Tanzania (pichani chini) ambayo alikabidhiwa hivi karibuni jijini Arusha.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages