NEWS

Monday 8 July 2024

Wito Mkali Kutoka kwa Viongozi wa Democratic: ‘Biden Aachane na Kampeni ya Urais’


Raisi wa Marekani Joe Biden
--------------------


Wabunge wengine kadhaa waandamizi wa chama cha Rais Joe Biden cha Democratic wamejiunga na wito wa kumtaka akabidhi ugombea wake katika uchaguzi wa Novemba kwa mgombea mwingine, vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti.

Wakati wa mazungumzo na Kiongozi wa walio Wachache Bungeni Hakeem Jeffries, wabunge wanne walizungumza wazi kumtaka Bwana Biden ajiondoe, kulingana na vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na mshirika wa BBC wa Marekani CBS News.

Wanne hao waliungwa mkono na wengine ambao walionyesha wasiwasi wao juu ya uwezo wa Bw Biden kuendelea kushikilia ofisi hiyo baada ya utendaji mbaya wa mjadala wa hivi majuzi, lakini hawakumuomba rais kujiondoa, CBS iliongeza.

Bw Biden ameapa kuendelea kuwa kinyang’anyironi, na amedumisha uungwaji mkono wa Wanademokrasia wengine ambao wanasisitiza kuwa yeye ndiye mtu atakayemshinda Donald Trump katika kura ya Novemba.

Maoni mbalimbali juu ya kugombea kwa Bw Biden yanatarajiwa kujitokeza zaidi siku ya Jumatatu baada ya wabunge kurejea Capitol Hill.


Rais pia ataangaziwa katika siku zijazo huku akiandaa mkutano wa kilele wa viongozi wa nchi za Nato huko Washington.

CHANZO: BBC

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages