NEWS

Wednesday, 7 May 2025

Kissu ateuliwa kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu



Shaaban Kissu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Africa Media Group, Shaaban Kissu, ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

Taarifa hiyo imetolewa leo Mei 7, 2025 na Katibu wa Rais, Waziri Salum, katika hafla ya chakula cha mchana kati ya Rais Samia na waandishi wa habari walioshiriki Tuzo za Samia Kalamu Awards jijini Dar es Salaam.

Kissu ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari, amepokewa taarifa hiyo ya uteuzi wake akiwa mshereheshaji katika hafla hiyo.
Read Also Section Example

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages