NEWS

Monday, 1 December 2025

Tume ya Uchunguzi matukio ya Uchaguzi Mkuu yataja mambo yatakayopewa kipaumbele

Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande Othman

 
Na Mwandishi Wetu

Tume ya Uchunguzi wa matukio ya vurugu zilizotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu 2025 imeanisha mambo sita yatakayochunguzwa.


Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande Othman, ameeleza katika taarifa yake kwa vyombo vya habari leo Desemba 1, 2025 kwamba eneo moja litakalochunguzwa ni kubaini chanzo halisi cha matukio hayo.


Amesema jambo jingine litakuwa kuchunguza lengo  lililokusudiwa na watu ambao tume itaona walipanga kutekeleza vitendo hivyo.


Tume hiyo pia itabainisha madhara yaliyojitokeza ikiwemo vifo, majeruhi, uharibifu wa mali na madhara ya uchumi na kijamii.


Tume hiyo pia itachunguza mazingira na hatua mbalimbali zilizochukuliwa na serkali na vyombo vyake na mtu mwingine yeyote.


Katika kukamilisha kazi, Jaji Mkuu Mstaafu Othman amesema tume yake itatoa mapendekezo ya maeneo yanayohitaji kuimarishwa ili kuongeza uwajibikaji kwa viongozi na raia katika kudumisha amani, utawala bora, haki za binadamu, utawala wa sheria hadi kufikia maridhiano kitaifa.


Mwishowe, tume hiyo itachunguza jambo lolote ambalo itaona linaendana na majukumu yake.

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages