NEWS

Wednesday 4 December 2019

MASHINDANO YA COPA COCACOLA KENYA




 Balozi wa Tanzania Nchini Kenya Dr Pindi Chana leo Novemba04,2019 ametia hamasa kubwa na kushuhudia  timu ya Copa cocacola Tanzania ikichuana na timu ya Copa cocacola ya Kenya katika shindano la nusu fainali lilofanyika  katika shule ya Mpesa Foundation Academy nchini Kenya.

Balozi  Dr Pindi Chana  amewapongeza vijana wa timu ya Copa cocacola ya Tanzania kwa kushiriki katika mashindano hayo ambayo fainali yake itafanyika kesho na kuhusisha pia timu ya Copa Coca cola ya Zimbabwe.


Akiongea na vyombo vya habari katika hafla hiyo, Balozi Dkt Chana amesema uwekezaji katika michezo kwa vijana sio tu ni muhimu kwa afya bali pia husadia kutengeneza ajira kwa vijana.
Balozi  Dr Chana pia amezipongeza nchi za Afrika kwa kuweka michezo kuwa sehemu ya masomo katika shule za sekondari .

                    

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages