NEWS

Friday 5 June 2020

IGP Sirro: Wanasiasa wasiingilie polisi, awatunuku vyeo askari Simiyu

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Simon Sirro, amewataka wanasiasa kufanya kazi zao kwa kufuata na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi bila kuingilia shughuli za kiutendaji za jeshi hilo.
IGP Sirro akiwatunuku vyeo Askari Polisi mkoani Simiyu


IGP Sirro ameyasema hayo Juni 3, 2020 wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Simiyu na kuongeza kuwa jeshi hilo halitawaingilia wanasiasa kwenye shughuli zao endapo hawatavunja sheria.

Amesisitiza kuwa jeshi hilo halitawavumilia wanasiasa wanaotumia nafasi zao kwenye vyama vya siasa kuingilia majukumu ya vyombo vya ulinzi na usalama.

Kamanda Sirro amewakumbusha wanasiasa watambua kuwa wanaendesha shughuli zao kwa sababu kuna amani na kwamba amani ikitoweka hawawezi kuziendesha, hivyo waliache jeshi hilo lifanye kazi yake kwa mujibu wa sheria za nchi.
IGP Simon Sirro akizungumza na askari polisi mkoani Simiyu
Katika hatua nyingine, June 4, 2020 IGP Sirro amewatunuku cheo cha koplo askari wawili wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU); ambao ni G 8018 Koplo Maiko Luvanda  na H 742 Koplo Paulo Komba na kuwapongeza kwa kazi nzuri waliyofanya na kuweza kutunukiwa vyeo hivyo.
Askari waliotunukiwa cheo cha koplo, G 8018 Koplo  Maiko Luvanda (kulia) na H 742 Koplo Paulo Komba
Kwa upande wao, askari hao walishukuru kwa kupandishwa cheo na kuahidi kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu na uamnifu pasipo kumuonea mtu yeyote.


(Imeandikwa na Anita Balingilaki, Bariadi)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages