NEWS

Wednesday 10 June 2020

SIMANZI: Mwalimu afa kwa moto Tarime

Mwalimu wa Shule ya Msingi Azimio ya mjini Tarime mkoani Mara, Richard Leonce amefariki dunia, huku mke na mtoto wake wakijeruhiwa vibaya kwa ajali ya moto iliyotokea nyumbani kwao leo Jumatano Juni 10, 2020, saa nne asubuhi.
Mwalimu Richard Leonce wakati wa uhai wake



Diwani wa Kata ya Bomani, Masubo Nkori na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa National, Bernard Nyagiro wameiambia Mara Online News kwamba mke wa Mwalimu Leonce, Happiness Mnisi ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Remagwe na mtoto wao wa kike, Bright, wamelazwa kwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime.

Kwa mujibu wa viongozi hao, chanzo cha ajali hiyo ya moto kinaweza kuwa hitilafu ya umeme ndani ya nyumba yao iliyopo eneo la National Housing mjini Tarime.

Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, ACP William Mkonda, amethibitisha na kusema jeshi hilo limeanza uchunguzi wa kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo ambayo pia imeteketeza mali mbalimbali zilizokuwa ndani ya nyumba ya familia hiyo.

(Imeandikwa na Samsn Chacha, Tarime)

1 comment:

  1. Kwa kweli nimeshtushwa sana na taàrifa ya ajali ya moto iliyosababosha Kifo cha rafiki yangu Mwl. Rich!

    Ee Mungu, utusaidie! Uwaponye majeruhi ( Mama na mwanawe)
    Àmen!

    ReplyDelete

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages