NEWS

Tuesday 14 July 2020

Mwenyekiti UVCCM Chuo cha Ushirika Moshi, Mwita Mohere avuta fomu ubunge Serengeti


Mwenyekiti UVCCM Chuo cha Ushirika Moshi,
Mwita Mhorere avuta fomu ubunge Serengeti
 MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi, Mwita Simion Mohere, leo Julai 14, 2020 amejitokeza kuchukua fomu ya kuwania ubunge katika jimbo la Serengeti mkoani Mara.
 Akizungumza na Mara Online News mara baada ya kuchukua fomu hiyo katika ofisi ya CCM Wilaya, Mohere amesema anahitaji kulistawisha kiuchumi jimbo la Serengeti ambalo anasema limekuwa nyuma kimaendeleo kutokana na kukosa mbunge mwenye uwezo na utashi wa kuwatumikia wananchi kwa kiwango kinachoridhisha.

“Serengeti tumekuwa nyuma kimaendeleo, nimeona nina uwezo na uzoefu wa uongozi, hivyo ninahitaji kuwa miongoni mwa viongozi wanaokwenda na kasi ya Rais Dkt John Pombe Magufuli katika kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli, mimi ni mtu sahihi, kwa uzoefu na uwezo wangu nina uhakika wa kuleta mabadiliko Serengeti,” amesisitiza Mohere.

1 comment:

  1. hakika huyu ndio mtu sahihi wa kulikomboa jimbo letu

    ReplyDelete

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages