NEWS

Tuesday 14 July 2020

Hezbon Peter Mwera afungua pazia fomu ya ubunge Tarime Mjini


MKURUGENZI wa Professor Mwera Foundation, Hezbon Peter Mwera(kulia), amekuwa mwanachama wa kwanza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuchukua fomu ya kuwani ubunge katika Jimbo la Tarime Mjini, leo asubuhi Julai 14, 2020.
 Kada huyo kijana na msomi wa chuo kikuu, amesema uwezo na uzoefu wake katika uongozi ndivyo vimemsukuma kuwania ubunge ili atumie nafasi hiyo kuharakisha maendeleo ya Tarime Mjini kwa kuhuisha miradi ya kijamii iliyosimama, kuboresha iliyopo na kuongeza mipya kwa manufaa ya wakazi wa jimbo hilo.
 Mwanachama wa CCM aliyemfuatia Mwera kuchukua fomu ya kinyang'anyiro hicho katika ofisi ya chama hicho wilaya ya Tarime ni Jackson Christopher Kangoye.

(Imeandikwa na Mara Online News)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages