Mwenyekiti wa UWT
Taifa, Mary Chatanda (katikati) akilia kwa uchungu baada ya kumtembelea mama aliyeokolewa
kwenye maafa ya mafuriko wilayani Hanang akiwa amejifungua mtoto wa kiume
salama.
NA MWANDISHI WETU, Hanang
---------------------------------------
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa, Mary Chatanda na msafara alioambata nao wamejikuta katika simanzi kubwa mara baada ya kumuona mama aliyejifungua saa chache baada ya kuokolewa kwenye tope lililomsomba mita kadhaa.
Akizungumza
wakati alipomtembelea mwanamke huyo juzi katika Kituo cha Afya Gendabi
wilayani Hanang, mahali yalipotokea maafa ya mafuriko na maporomoko ya
tope kutoka Mlima Hanang.
"Nimeshindwa
kujizuia mimi kama mama nikajikuta nalia kwa uchungu kuona mwanamama huyu
ambaye alisombwa na tope na kuweza kuokolewa kwenye tope hilo na
kufikishwa hospitali masaa mawili baadaye akajifungua salama mtoto wa
kiume,” alisema Chatanda na kuendelea:
“Kwa
kweli nimelia uchungu baada ya kusikiliza simulizi za mama huyu namna
alivyohangaika kuokoa watoto wake wawili na huku mjamzito wa miezi tisa, hakika
hakuna kama mama. Namshukuru sana Mungu kutenda maajabu na kumwezesha mama huyu
kujifungua salama na mtoto yupo salama na ameitwa Mussa."
Aidha, Mwenyekiti huyo wa UWT Taifa, alisema jumuiya hiyo ya chama tawala - CCM itafanya jitihada kuhakikisha wanamuimarishia mahitaji mama huyo ambaye kwa sasa na familia yake wanalala hospitalini kutokana na makazi yao kuharibiwa na mafuriko yaliyoambatana na tope.
No comments:
Post a Comment