
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan
Na Mwandishi Wetu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan amemteua James Wilbert Kaji kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt Moses Kusiluka na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Sharifa Nyanga.
Kabla ya uteuzi huo, Kaji alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Basi la Kisire lapata ajali Magu, baadhi ya abiria wahofiwa kufa
>>Vinicius Jr ashinda Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa FIFA
>>Musoma Vijijini: Wazazi CCM wamtunuku Prof Muhongo Tuzo ya ‘Uchaguzi wa Serikali za Mitaa’
>>TAMISEMI yatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2025
No comments:
Post a Comment