NEWS

Saturday 27 July 2019

MARA DAY KUFANYIKA SERENGETI, SEPTEMBA 15



Wanafunzi wakiimba nyimbo za uhifadhi katika sherehe za maadhimisho ya siku ya mto Mara iliyofanyika Tanzania kwa Mara ya Kwanza , Mugumu Serengeti Septemba 15 ,2013
Na Mwandishi wetu, Serengeti
Sherehe za maadhimisho ya   siku ya Mto Mara mwaka huu zitafanyika nchini Tanzania Septemba 15  katika Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara .
 Tayari tumenaza maandalizi  na tunategemea  kupata wageni wengi kutoka  ndani na je ya nchi  watakaohudhuria  sherehe siku hii muhimu ,  Mkuu wa Wilaya ya Serengeti(DC) Nurdin Babu ameiambia Mara Online leo .
Tanzania na Kenya huadhimisha siku ya  mto Mara September 15 kila mwaka kwa kupokezana. ikiwa ni sehemu ya kuendeleza  juhudi za uhifadhi endelevu katika bonde la mto  huo .
Sherehe hizo zilifanyika Bomet  nchini Kenya mwaka jana .

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages