NEWS

Wednesday 9 October 2019

8 WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA WIZI WA DHAHABU NORTH MARA


Na Mwandishi wetu,
Watuhumiwa 8 waliokamatwa wakiiba mawe ya dhahabu yenye thamani ya zaidi ya milioni 200 ndani ya mgodi wa North Mara hivi karibuni leo Oktoba 9, 2019 wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Tarime na kusomewa mashitaka matano ikiwemo shitaka la uhujumu uchumi na utakatishaji fedha.
Watuhumiwa hao ni Zabroni John Seth, James Mahalareri Makune, Jonathan Chuwa Genji,Amos Raphael Wahere, Mseti Chacha Isaka, Chacha Marwa Ryoba, Petro Kegora Mariba na Samson Mathoyo Leonard.

Wakati huo huo Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo leo amezungumza na waandishi wa habari mjini Tarime  na kuonya wale wote wanaoshiriki kufanya wizi wa mawe ya dhahabu katika mgodi North Mara  kuacha mara moja.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages