NEWS

Wednesday 16 October 2019

YANGA YAANZA KUWAPA PRESSURE WAARABU WA MISRI









 
Neema  imerejea  Yanga kufuatia kurejea kwa wachezaji wake watano waliokuwa majeruhi baada ya kuanza mazoezi mepesi juzi Jumatatu.

Wachezaji hao walianza mazoezi wakiwa katika program maalum wakati kikosi cha timu hiyo kikiwa dimbani kucheza dhidi ya Friends Rangers ambayo ililala kwa mabao 4-2.

Mrisho Ngassa, Patrick Sibomana, Paul Godfrey 'Boxer', Lamine Moro na Sadney Urikhob ndiyo wachezaji waliokuwa wakifanya mazoezi hayo wakati mechi inaendelea.



Kurejea kwa wachezaji hao kumeanza kutia morali kwa Yanga ambayo itakabiliana na Pyramids FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika Oktoba 27 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages