NEWS

Sunday 29 March 2020

Corona: Halmashauri Serengeti sasa inawapima abiria wanaoingia na kutoka


HALMASHAURI ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara kupitia hospitali ya wilaya hivi sasa inawafanyia vipimo vya joto  abiria wa mabasi na magari ya watu binafsi wanaoingia na kutoka wilayani humo kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Shughuli hiyo inaendeshwa na wataalamu wa afya katika lango la Fort Ikoma la kuingia na kutoka ndani ya hifadhi hiyo chini ya usimamizi wa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti(DMO), Dkt Emiliana Donald.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mhandisi Juma Hamsini amesema mpango huo utakuwa endelevu kipindi hiki cha janga la Corona kuhakikisha usalama wa afya za abiria wanaosafiri kupitia ndani ya hifadhi hiyo kuelekea Ngorongoro, Manyara, Karatu na Arusha.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages