NEWS

Sunday 22 March 2020

Rais Magufuli: Corona isitufanye tumsahau Mungu


 RAIS wa Tanzania Dkt John Magufuli amesema kuwepo kwa ugonjwa wa Corona isiwe sababu ya watu kutishana kiasi cha kumsahau Mungu.

Badala yake, Rais Magufuli amewataka Watanzania kuendelea kuchapa kazi na kujenga uchumi huku wakizingatia maelekezo ya kitaalamu ya kujikinga nao na kumwomba Mungu auepushe.
 Aidha, amekemea tabia ya watu wanaofanya mzaha juu ya ugonjwa huo na kuwatia hofu wananchi kupitia mitandao ya kijamii.
 Akizungumza katika ibada ya Jumapili leo kwenye Kanisa la Mtakatifu Paulo wa Msalaba Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma iliyoongozwa na Paroko wa Parokia hiyo, Padre Onesmo Wisi, Rais Mgufuli amesema:“Watu tusitishane, tunatishana mno. Niwaombe ndugu Wakristo na Watanzania kwa ujumla na madhehebu yote, huu ndio wakati mzuri sana wa kumtegemea Mungu kuliko wakati wote, tuendelee kuchapa kazi, tuendelee kujenga uchumi wetu, hatuwezi kusalimu amri kwa ugonjwa huu wa Corona na kushindwa kumtegemea Mungu.”


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages