NEWS

Sunday 26 April 2020

Mafuriko Ziwa Victoria: RC Mara atahadharisha wavuvi


Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mara, Adam Malima, hivi karibuni amefanya ziara katika mwalo wa Sota wilayani Rorya na kuwataka wavuvi kuwa makini dhidi ya ongezeko kubwa la maji katika Ziwa Victoria.
Tayari watu wawili kutoka eneo hilo wanahofiwa kufa maji wakivua samaki ziwani humo.

Hivi karibuni ofisi ya Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria (LVBWB) ilitoa tahadhari baada ya kubaini kina cha maji katika ziwa hilo kimeongezaka hadi kufikia mita 1134.47 kutoka usawa wa bahari.
Watalaamu wanasema kiwango hicho cha maji kimevunja rekodi kwani hakijawahi kufikiwa katika kipindi cha miaka 55 iliyopita.


Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima (kushoto), akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa huo katika eneo la Sota wilayani Rorya.

Aidha, Mkuu wa Mkoa, Malima, ametawaka wavuvi kutotumika kuvusha wageni kuingia nchini kiholela, hasa kipindi hiki cha mlipuko wa janga la COVID-19 linalosababishwa na virusi vya corona.

Amewandoa hofu wavuvi hao dhidi ya vitendo vya utekwaji wakiwa katika shughuli zao akisema serikali itaendelea kuimaisha doria katika ziwa hilo.
Askari polisi wa kikosi cha maji wakiwa kazini eneo la Sota, Rorya.

Lakini ametawaka kufanya uvuvi upande wa Tanzania na kuacha tabia ya kuvuka mipaka.

Ziwa Victoria linazungwaka na nchi tatu za Afrika Mashariki; ambazo ni Tanzania, Uganda na Kenya.

(Habari, picha zote na Mussa John, Rorya)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages